MTUMAINI BWANA NYAKATI ZOTE

MTUMAINI BWANA NYAKATI ZOTE. ISAYA 40:28 – 31; ZABURI 62:8

  • Kutumaini– kuwa na Imani, kutegemea, kuwa na uhakika juu ya mtu au jambo fulani.
  • Kumtumaini Bwana –  kumwamini na kumtegemea
  1. MUNGU NI WA MILELE NA MWENYE UWEZA WOTE
    Isaya 40: 27 – 28; zaburi 90:2; 62:8

Key verses

Isaya 40:28 Je! Wewe hukujua? Hukusikia? Yeye Mungu wa milele, BWANA, Muumba miisho ya dunia, hazimii, wala hachoki; akili zake hazichunguziki.

Zaburi 90:2 Na tangu milele hata milele ndiwe Mungu.

2. MUNGU HUWAPA NGUVU WALIOCHOKA NA WANYONGE. Isaya 40:29 

Key verse Isaya40:29. Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo.

Waliochoka – nguvu zimekwisha, waliolemewa na mizigo, waliokata tamaa kwa sababu ya changamoto mbalimbali.

  • Eliya – alikata tamaa na kuomba Mungu amuue. (1Fal 19:1 – 8)
  • Mungu akamtia nguvu aendelee mbele.

Wanyonge/dhaifu – wasiokuwa na uwezo au nguvu.

  • Gideon – alijiona dhaifu, hastahili, sio shujaa.
  • Mungu akampa jina “shujaa, Hodari.”
  • Mungu alimpa nguvu na ushindi.

3. NGUVU ZA MUNGU HUWEZESHA WATU WAKE KUSHINDA CHANGAMOTO 

Isaya 40:30 – 31; Ayubu 19: 19 – 20; 25 – 26

Key verses. Isaya 40: 31 bali wao wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watakimbia, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.

Ayubu 19:25 Lakini mimi najua ya kuwa Mteteaji wangu yu hai, Na ya kuwa hatimaye atasimama juu ya nchi.

Join the Discussion

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top