SIKU 21 ZA MAOMBI NA KUFUNGA IJUMAA 16 JANUARI 2026.
🙏 MAOMBI KWA AJILI YA JAMII YETU 🙏
Leo tunasimama kidete kuwaombea wale walio karibu nasi na wenye uhitaji maalum. Ungana nasi katika mambo haya manne:
1️⃣ Wenye Uhitaji Maalum: Tuwaombee Wazee, Wajane, Yatima, na Walemavu. Mungu akutane na mahitaji yao ya kila siku. 📖 Zab 145:14-16, Eze 22:30, Mit 31:20
2️⃣ Kanisa Kuhudumia Jamii: Tuombe Mwili wa Kristo upate neema ya kuwagusa wahitaji kwa utukufu wa Mungu. 📖 Kum 15:11, Mit 14:31
3️⃣ Mungu Akutumie Wewe: Omba Mungu akufanye kuwa chombo cha baraka kwa jamii inayokuzunguka. Usipite pembeni, kuwa jibu la maombi yao. 📖 Mit 22:2, 21:13
4️⃣ Shukrani kwa Wanaojitoa: Tunawashukuru na kuwaombea watu wote na vikundi vinavyojitoa kuhudumia jamii kwa hali na mali. 📖 Yakobo 1:27, Mdo 20:35

