Maombi ya Katikati ya Mwaka – Maombi ya Shukrani Jumatatu, 13 Julai 2026

๐Ÿ™ย MAOMBI YA KUFUNGA NA KUOMBA NUSU MWAKA
Jumatatu, 13 Julai 2026

Tunakukaribisha kuanza wiki hii ya kufunga na kuomba kwa kumtafuta Mungu kwa moyo wote. Tuungane katika maombi tukimshukuru Mungu kwa uaminifu wake na kumkabidhi nusu ya pili ya mwaka 2026 mikononi mwake.

๐Ÿ•Š๏ธ 1. Maombi ya Shukrani
๐Ÿ“– Zaburi 103:1โ€“5; 1 Wathesalonike 5:16โ€“18

  • Mshukuru Mungu kwa kutuvusha salama nusu ya kwanza ya mwaka 2026.
  • Mshukuru kwa maisha yako, familia yako, kazi yako, na baraka zake nyingi.
  • Mshukuru kwa ajili ya Kanisa lake.
  • Mshukuru kwa ajili ya Taifa la Tanzania na ulimwengu mzima.

๐Ÿ™Œ 2. Mkabidhi Mungu Nusu ya Pili ya Mwaka 2026
๐Ÿ“– Mithali 3:5โ€“6; Zaburi 37:5; Isaya 43:18โ€“19

  • Mwombe Mungu akuongoze, akufungulie milango mipya, na akatimize makusudi yake katika maisha yako.

๐Ÿ™ 3. Ombea Mahitaji ya Wiki Hii
๐Ÿ“– Wafilipi 4:6โ€“7; Yeremia 33:3

  • Wasilisha mbele za Mungu mahitaji yako binafsi, ya familia, Kanisa, na Taifa, ukiamini kuwa Yeye husikia na kujibu maombi.

“Mkabilieni Mungu kwa imani, kwa maana Yeye ni mwaminifu na anaweza kufanya mambo mapya.”

#MidYearPrayerAndFasting #MaombiYaKufunga #DPCKinondoni #PrayWithoutCeasing #TrustTheLord #DarEsSalaamPentecostalChurch #Tanzania

Join the Discussion

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top