SIKU 21 ZA MAOMBI NA KUFUNGA SIKU YA 12

SIKU 21 ZA MAOMBI NA KUFUNGA IJUMAA 16 JANUARI 2026.
🙏 MAOMBI KWA AJILI YA JAMII YETU 🙏

Leo tunasimama kidete kuwaombea wale walio karibu nasi na wenye uhitaji maalum. Ungana nasi katika mambo haya manne:

1️⃣ Wenye Uhitaji Maalum: Tuwaombee Wazee, Wajane, Yatima, na Walemavu. Mungu akutane na mahitaji yao ya kila siku. 📖 Zab 145:14-16, Eze 22:30, Mit 31:20

2️⃣ Kanisa Kuhudumia Jamii: Tuombe Mwili wa Kristo upate neema ya kuwagusa wahitaji kwa utukufu wa Mungu. 📖 Kum 15:11, Mit 14:31

3️⃣ Mungu Akutumie Wewe: Omba Mungu akufanye kuwa chombo cha baraka kwa jamii inayokuzunguka. Usipite pembeni, kuwa jibu la maombi yao. 📖 Mit 22:2, 21:13

4️⃣ Shukrani kwa Wanaojitoa: Tunawashukuru na kuwaombea watu wote na vikundi vinavyojitoa kuhudumia jamii kwa hali na mali. 📖 Yakobo 1:27, Mdo 20:35

Maombi #JamiiYetu #UpendoWaKristo #WenyeUhitaji #MaombiYaLeo

Join the Discussion

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top