SIKU 21 ZA KUOMBANA KUFUNGA SIKU YA 13

SIKU 21 ZA KUOMBANA KUFUNGA – JUMAMOSI 15, 2026

OMBI KUU: USHIRIKA WENZA NA USHIRIKIANO

1. Maombi binafsi

• Mshukuru Mungu ushirikiano mzuri ulionao na familia yako.

• Mshukuru Mungu kwa mahusiano mazuri na watu wengine katika maisha ya kila siku – waamini wenzako, wafanya kazi wenzako, majirani Mithali 27:17.

• Omba utulivu, umoja, mshikamano na upendo katika familia yako 

Isaya 32:18; Wakolosai 3:15

2. Mshukuru Mungu kwa kukupa nafasi ya kuhudumia wengine.

• Mshukuru Mungu kwamba amekuwezesha kuwahudumia wengine kiroho, kimwili na kijamii Mathayo 5:9; 25:34 – 36 

• Mshukuru Mungu kwa kukuwezesha kushiriki katika kazi ya Bwana kupitia kanisa la DPC Wafilipi 1:3 – 5 

• Omba kwamba Mungu aendelee kukutumia kwa ajili ya utukufu wake Wafilipi 1:6 

3. Mshukuru Mungu kwa ushirika wa DPC na makanisa mengine.

• Mshukuru Mungu kwa ushirikiano wa PAOC katika kuwezesha kazi ya Mungu Tanzania na Africa.

• Omba kwama kanisa la Tanzania ikiwemo PAGT litaendelea kukua kihuduma na kuyafikia mataifa mengine Mathayo 28:19 – 20 

• Omba kwa ajili ya Mwanza Christian College kiweze kuandaa watumishi wengi wa injili Waefeso 4:11 – 13

4. Omba kwa ajili ya makanisa yote ambayo yamejitoa kuhubiri Injili ya Kristo.

• Ombea CPCT (Council of Pentecostal ChurchesT in anzania) waweze kutimiza kusudi la Mungu katika makanisa ya kipentecoste 1Kor 12:4 – 6

• Omba roho ya ushirikiano katika kupeleka injili kwa wale ambao hawajafikiwa Warumi 12:14 – 15 

5. Ombea ibada za Jumapili – Omba uwepo wa Mungu na nguvu za Roho Mtakatifu.

Join the Discussion

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top