MWONGOZO WA MAOMBI –  IBADA YA KUSIFU NA KUABUDU YA MWISHO WA MWEZI JUNI 2022

A. SHUKRANI NA SIFA KWA MUNGU (1 Nya 16:7-9, Zab 95:1-6; 34:1-3, 2 Kor 2:14.)

● Mshukuru Mungu:-

~ Kwa ajili ya wema wake na uaminifu wake kwako na wote wanaokuzunguka.

~ Ushindi aliotupa katika nusu hii ya kwanza ya mwaka, kibinafsi na kama kanisa (Januari hadi Juni).

~ Kwa neema, upendo, fadhili, wema na rehema zake juu ya kanisa letu.

~ Kwa ajili ya huduma  unayohudumu kanisani (Kumpenda Mungu, nguvu ya kutumika, umoja na amani katika timu yako).

B. TOBA NA UTAKASO (Mit 28:13, Zab 32:5; 139:23-24, Ufu 5:9-10.)

● TUBU

~ Muombe Roho Mtakatifu auchunguze moyo wako na akusemeshe juu ya dhambi yoyote inayokupasa kuitubia.

~ Mahali tulipomtumikia chini ya viwango.

~ Tubu kwa niaba ya timu yako, wote watakaohudumu, kanisa na kusanyiko zima.

~ Mshukuru Mungu kwa msamaha na rehema zake kwetu.

C. HUDUMA NZIMA (Zab 40:8; 32:8, 1 Sam 15:22, 2 Sam 5:3, Isa 40:29, Mdo10:38.)

● KWA AJILI YAKO NA WOTE WATAKAOHUDUMU 

☆ OMBA;

~ Roho Mtakatifu akufunulie kusudi na mapenzi yake kwa ajili ya ibada.

~ Maelekezo na uongozi wa Roho Mtakatifu katika maandalizi yetu.

~ Neema ya kumtumikia kwa uaminifu na ufanisi.

~ Nguvu; kiroho, kimwili, kiakili na kihisia.

~Upako mpya na wa kiwango kingine uwe juu yetu, Bwana anavyotutumia kufanya kile alichokikusudia katika ibada hii.

~ Moyo wenye kutii sauti ya Roho Mtakatifu ili tukae katika mapenzi yake wakati wote wa huduma.

~ Umoja katika roho.

● MNENAJI WA NENO (Isaya 40:8, Luka 24:45; 22:42b na 4:14, 22, 32.)

☆ OMBEA:-

~ Mnenaji kubeba ajenda ya Mungu na kutoa neno la wakati.

~ Mamlaka, ujasiri na ufasaha katika kulinena neno.

~ Tamka, utimilifu wa neno la Mungu na kusudi lake kwa wale watakaolisikia; liguse maisha, hali zao na mambo wanayoyapitia.

● KUSANYIKO (Yer 30:19, Ebr 11:1-2 na 6, Mdo 2:1-2, 2 Nya 5:13.)

☆ OMBEA:-

~ Mioyo iliyojaa shukrani kwa Mungu kwa yote aliyofanya katika nusu hii ya kwanza ya mwaka, na yale ambayo bado hajafanya.

~ Imani ya kupokea kile ambacho wamekuwa wakimwamini Mungu kuwatendea na matarajio yao kwa nusu ya pili ya mwaka.

~ Udhihirisho wa uwepo wa Mungu, upako na nguvu za Roho Mtakatifu ili kutimiza kusudi la kila mtu binafsi katika miezi sita ijayo.

D. KIRI NA KUTANGAZA (Isa 2:3, Yoh 4:28-30, Luka 4:18 &19, 2Kor 10:4-5, Isa 54:14-17, Zab 91.)

Tamka:-

~ Mahudhurio; mitandao ya kijamii na njia nyingine za kueneza habari; zibebe upako wa Roho Mtakatifu, na kwamba kila ambaye Mungu amemkusudia kuja atakuja, na wale watakaoabudu kwa njia ya mtandao watahudumiwa.

~ Juu ya wahudhuriaji wote;

☆ Wokovu

☆ Uponyaji

☆ Upenyo

☆ Kufunguliwa

☆ Urejesho

☆ Uamsho

~ Damu ya Yesu ikufunike wewe na wapendwa wako wote tunapoendelea kujiandaa na ibada.

☆ Kila mpango wa adui na kila silaha itakayoinuka kinyume na wewe haitafanikiwa.

*Hakuna ugonjwa.

*Hakuna ajali.

*Hakuna kufa kabla ya wakati.

Join the Discussion

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top