MWONGOZO WA MAOMBI YA IBADA YA KUSIFU NA KUABUDU APRILI 2023

MWONGOZO WA MAOMBI  APRILI 2023.

DHIMA: NGUVU NA UFUNUO WA KAZI YA MSALABA. (WAKOLOSAI 2:14-15)
TAFSIRI ZA BIBLIA (NIV, NKJV, KJV, AMP, AMPC, SUV, NENO).

1). SHUKRANI KWA MUNGU WETU.

● Kwa ajili ya upendo wake, Rehema na Uaminifu. 1Yohana 4:19, Waefeso 2:4-5, Yohana 3:16.

● Mshukuru Mungu kwa kazi iliyokamilika ya MSALABA. Yohana 19:30.

Kupitia Msalaba…

  ~Tulipokea zawadi ya Wokovu (Uzima wa Milele)

  ~Nguvu ya dhambi, mauti na kaburi imevunjwa. Warumi 6:11, 

1 Wakorintho 15:55 na Ufunuo 1:18.

  ~ Tumesamehewa, tumehesabiwa haki, tumetakaswa, tumekombolewa, tumefunguliwa na kupatanishwa naye.

  ~ Tumepona. Isaya 53:4-5.

  ~ Sisi ni washindi. Wakolosai 2:14-15, 1Wakorintho 1:18

  ~ Tumepata utambulisho mpya katika Kristo. Kanisa limepewa nguvu na mamlaka. 

Waefeso 2:6.

~ Tumefanywa kuwa wafalme na makuhani, na tunamiliki na kutawala juu ya nchi. 

(Ufunuo 5:9-10).

  ~Tunajifunza nguvu ya kudumu katika maombi (uwezo wa kukaa katika maombi hadi kuzaa kitu na kupata ushindi) na kuvumilia mpaka mwisho. Luka 22:39-46 .

 2). TOBA NA HUDUMA.

 (Jiombee na kuombea wengine hasa katika huduma unazotumika).

● Mkaribie Mungu kwa toba.

Omba damu yake ya thamani itusafishe, itufanye safi kwa ajili ya matumizi ya Bwana wetu.

Zaburi 24:3-4, 1Timotheo 2:8, Waebrania 9:14 na 2Timotheo 2:20-21.

● Tubu kwa niaba ya wahudumu wote na kusanyiko zima. Ufunuo 1:5-6.

●Jiombee na ukabidhi mahitaji yako kwake. Wafilipi 4:6. Mshukuru kwa sababu atatukumbuka na sisi tunapofanya kazi yake. Waebrania 6:10.

●Omba nguvu za kutumika, nguvu za Mungu zifanye kazi ndani yetu, hekima ya kutuongoza, kufanya kila kitu kwa ubora na kujitoa katika yote tunayofanya. Muhubiri 10:10, Waefeso 6:7-8.

● Tamka kwamba:- Tutafanya kazi alizofanya Kristo na zaidi. 1Yohana 3:8, Yohana 14:12.

3).IBADA NZIMA.

● Ombea:-

   ~Mioyo yenye matarajio, iliyojaa imani ya kupokea kutoka kwa Mungu. Marko 11:22-24.

   ~Watu wa Mungu wapate ufunuo mpya wa jina la YESU na JINA LA YESU linene na hali zao. Wafilipi 2:5-11, Matendo 4:12 ; 2:22 ; 3:1-16.

    ~ Watu wa Mungu wapate ufunuo mpya wa kazi iliyokamilika ya msalaba. 1 Wakorintho 1:18; 15:58, Wagalatia 3:13-14, Wakolosai 1:13-14.

   ~Mapenzi na kusudi la Mungu katika maandalizi yetu yote hadi siku ya mwisho. 

Mathayo 6:10, Zaburi 135:6.

   ~ Udhihirisho wa uwepo wa Mungu na nguvu ya JINA LA YESU tunapokusanyika pamoja. Mathayo 18:20, Matendo 2:1-18, Luka 10:17.

   ~Ombea mnenaji wa neno.

        *Mkabidhi Mungu maandalizi yote ya mnenaji. Mithali 16:1

*Omba upako wa kuhubiri neno. Usemi wake; Mungu ampe neno la majira kwa ajili ya watu wake nalo likatimize kusudi lake. 

Omba wokovu wa roho na uamsho. 

1 Wakorintho 1:4-5; 2:4-5, Luka 4:18-19.

     *Ombea udhihirisho wa wana uamsho wa nyakati za mwisho ili kuhubiri Injili. Warumi 1:16, Mathayo 9:37-38.

● Tamka:

   *MBINGU IMEFUNGUKA kwenye eneo la DPC. (Luka 3:21).

  *Watu wengi waje kula mezani pa Mungu Jumapili hii na kusiwe na cha kuwazuia.

4). INUA JINA LA YESU KUPITIA SADAKA YA SIFA.

●Jina la Yesu linapoinuliwa kupitia dhabihu ya sifa, MWINULIE YESU SHANGWE:-

   * Kwa ajili ya miujiza, ishara na maajabu. Matendo 2:22.

  * Kwa uponyaji. Matendo 10:38

  * Kufunguliwa.

  * Kupigana vita yako. Zaburi 27:2-3.

  * Kupigana na watesi wako. Zaburi 35:1

  * Kwa urejesho.

  * Kuokoa wapendwa wako. Mathayo 1:21.

● Kiri na kutamka kwamba;-

    ~Yesu anazo funguo za mauti na kuzimu (Ufu 1:18), kwahiyo milango ya kuzimu haitatushinda sisi, maandalizi yetu wala ibada. Mathayo 16:18.

   ~ Tamka Isaya 41:11-13, Zaburi 35:1-10 na 121, juu yako mwenyewe, timu yako ya huduma, wapendwa wako na ibada nzima.

Join the Discussion

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top